• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Mume ameniruhusu nitafute madume wa kumsaidia kazi, demu afunguka

Mume ameniruhusu nitafute madume wa kumsaidia kazi, demu afunguka

Na JANET KAVUNGA

BAMBURI, MOMBASA

MWANADADA aliyeolewa hapa aliacha wenzake midomo wazi alipowaambia kwamba mumewe amemhurusu awe akiburudishana na wanaume wengine.

Demu huyo alidai hapati raha ya kutosha katika ndoa yake.

Demu alifichua haya kwenye gumzo na wenzake baada ya mkutano wa chama.

“Msijifunge mkikosa raha katika ndoa zenu. Niliambia mume wangu aniruhusu niwe nikiburudishwa na wanaume wengine kwa kuwa hanitoshelezi na hangekataa kwa kuwa hana uwezo wa kushughulikia hanjam zangu kikamilifu,” demu alifunguka.

Baadhi ya wenzake hawakuamini lakini akasisitiza kuwa hawezi kusononeka katika ndoa kwa kukosa raha ilhali kuna wanaume magwiji wanaoweza kumshughulikia.

“Haufanyii haki ndoa yako na unafaa kuiheshimu,” mwanadada mmoja alimwambia.

  • Tags

You can share this post!

MAWAIDHA YA KIISLAMU: Fadhila za ugonjwa kwa Muislamu ni...

Mwanamuziki Dennis Mutara hatimaye aruhusiwa kuondoka...

T L