• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Aliyetaka kula tunda kwa nguvu ameomba msamaha akitaka turudiane

Aliyetaka kula tunda kwa nguvu ameomba msamaha akitaka turudiane

SHANGAZI;

Kuna mwanamume aliyekuwa mpenzi wangu lakini nikamchukia na kumuacha alipotaka kunilazimisha tushiriki mahaba. Sasa amerudi kwangu akiomba turudiane. Nipe ushauri.

Hatua ya mwanamume huyo ni ishara kuwa anakupenda kwa dhati na hataki kukupoteza. Kama bado unampenda, mkubali na umwelezee jinsi unavyotaka muendeshe uhusiano wenu.

Miaka 15 sijapata mke, nimerogwa?

Nilianza kutafuta mke nikiwa na miaka 30 na kufikia sasa sijafanikiwa ingawa nina miaka 45. Tatizo ni kuwa kila mwanamke tunayependana huniacha baada ya muda mfupi tu. Je, nimerogwa nisipate mke?

Siamini mambo ya ushirikina. Hata hivyo, huo ni muda mrefu sana wa kutafuta ilhali kuna wanawake wengi wanaotamani kuolewa. Labda una udhaifu fulani unaowafanya wakuache. Jaribu kuwauliza waliokuacha uone kama watakwambia.

Ghafla ameanza kudai tutumie kinga chumbani

Nimekuwa na mpenzi kwa miaka miwili. Tumekuwa tukifurahia burudani bila kinga kwa sababu kuna mbinu nyingine tunayotumia kuzuia mimba. Sasa ghafla ameanza kusisitiza tutumie kinga. Simuelewi, nishauri.

Mpenzi wako ana sababu nzuri ya kusisitiza mtumie kinga. Labda anashuku una mwingine na hawezi kukwambia kwa sababu hana ushahidi. Kama sivyo, ndiye anayekucheza na anataka kukukinga.

Mchumba wa miaka 5 ataka tuoane lakini kwa kweli sina hisia kwake

Mchumba wangu wa miaka mitatu ananipenda sana na ameamua kunioa. Ajabu ni kuwa nimepoteza hisia kwake. Hali hiyo inanisumbua kwa sababu sitaki kuolewa na mtu nisiyempenda. Nifanye nini?

Itakuwa vigumu kumshawishi mpenzi wako kuwa huna hisia kwake ilhali mmekuwa wapenzi kwa miaka mitatu. Atavunjika moyo sana akijua ukweli huo. Lakini itabidi umwambie tu liwe liwalo.

  • Tags

You can share this post!

‘Cherera 4’ waibuka wakishikilia kura ya 2022...

Mjane, 64, alivyokita katika ushonaji kofia kukabili upweke...

T L