Na WACHIRA MWANGI
KATIBU wa Wizara ya Mawasiliano na Vijana, Bi Esther Koimett (pichani), ameonya vijana kuwa watajuta kwa muda mrefu iwapo hawatafanya maamuzi ya busara katika uchaguzi ujao.
Akizungumza Mombasa, katibu huyo aliwashauri vijana wahakikishe watachagua viongozi ambao hawatatatiza amani ya nchi na kuvuruga hali ya kufanikisha maendeleo.
Alikuwa amehudhuria hafla ya kuzindua kitabu kilichoandikwa na Waziri Msaidizi Nadia Abdalla.
“Tuna nafasi kubwa ya kufanya maamuzi ya uongozi bora kuanzia kwa wadi, kaunti, maeneobunge hadi urais,” akasema.