Na ALEX KALAMA
GAVANA wa Kaunti ya Kilifi, Bw Amason Kingi, ameitaka serikali ya kitaifa iharakishe ukarabati wa daraja la Buntwani, eneo la Malindi.
Akizungumza katika Wadi ya Shella wikendi, alisema serikali ya kitaifa ilisisitiza ukarabati huo si jukumu la kaunti.
Gavana huyo aliihimiza serikali kuu kukamilisha ujenzi wake akiongeza kuwa jinsi lilivyo, linahatarisha maisha ya watu wanaozuru eneo hilo.