• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Ashtakiwa kumsababishia kero jirani akimshuku kanasa mume wake

Ashtakiwa kumsababishia kero jirani akimshuku kanasa mume wake

NA ESTHER NYANDORO

MWANAMKE anayedaiwa kumdhulumu jirani yake akimshuku kuwa aliiba mumewe na kumfilisi amefunguliwa mashtaka ya kuzua fujo na kusababisha ukosefu wa amani.

Bi Eunice Moraa anashtakiwa kwa kutenda kosa hilo mnamo Machi 13, 2022 katika eneo la Southlands mtaani Langata, Kaunti ya Nairobi.

Ripoti ya uchunguzi wa polisi inasema kuwa kosa hilo lilitokea baada ya mabishano mafupi kuzuka kati ya mwanawe mshtakiwa na jirani yake walipokuwa wakichota maji.

Mahakama iliambiwa mtoto huyo wa mshtakiwa alienda nyumbani kwao na kutoa taarifa kwa mama yake na hapo wakaandamana mpaka kwa nyumba ya mlalamishi.

Mahakama imeambiwa ni hapo ndipo mshtakiwa alisababisha mazingira ya ugomvi na majibizano makali.

Kesi hiyo iliripotiwa kwa wazee wa kijiji ambao waliingilia kati lakini Moraa alikataa kulipa ndoo kama walivyokubaliana na kisha akaripotiwa kwa polisi.

Hata hivyo alikanusha mashtaka mbele ya Hakimu Mkuu Mwandamizi Phillip Mutua.

Bi Moraa aliachiliwa kwa dhamana ya Sh20,000 pesa taslimu na mdhamini wa kiasi sawa na hicho.

  • Tags

You can share this post!

White Cap yadhamini mbio za magari za akina dada pekee...

Kamati ya kufuatilia shughuli za uchaguzi Pwani yazinduliwa

T L