• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Kamati ya kufuatilia shughuli za uchaguzi Pwani yazinduliwa

Kamati ya kufuatilia shughuli za uchaguzi Pwani yazinduliwa

NA KNA

KAMISHNA wa eneo la Pwani, Bw John Elungata (pichani), amezindua kamati inayoleta pamoja wadau mbalimbali wa masuala ya uchaguzi.

Kamati hiyo inajumuisha wawakilishi kutoka kwa idara za usalama, serikali za kaunti, mashirika ya kijamii, wafanyabiashara na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).

Hatua hiyo inatarajiwa kusaidia kuendesha shughuli za kuwezesha uchaguzi wa amani na haki utakaoshirikisha wananchi wote.

Akizungumza Mombasa, Bw Elungata alitaka wanasiasa wakemee wazi ghasia za uchaguzi akisisitiza kuwa uchaguzi haufai kuwa makabiliano ya ‘kufa kupona’.

  • Tags

You can share this post!

Ashtakiwa kumsababishia kero jirani akimshuku kanasa mume...

Jinsi makaa spesheli yanavyosaidia kupunguza gharama ya...

T L