NA KNA
KAMISHNA wa eneo la Pwani, Bw John Elungata (pichani), amezindua kamati inayoleta pamoja wadau mbalimbali wa masuala ya uchaguzi.
Kamati hiyo inajumuisha wawakilishi kutoka kwa idara za usalama, serikali za kaunti, mashirika ya kijamii, wafanyabiashara na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC).
Hatua hiyo inatarajiwa kusaidia kuendesha shughuli za kuwezesha uchaguzi wa amani na haki utakaoshirikisha wananchi wote.
Akizungumza Mombasa, Bw Elungata alitaka wanasiasa wakemee wazi ghasia za uchaguzi akisisitiza kuwa uchaguzi haufai kuwa makabiliano ya ‘kufa kupona’.