• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 11:39 AM
Ashtakiwa kwa kushirikiana na rafikiye kudhulumu dadake kimapenzi

Ashtakiwa kwa kushirikiana na rafikiye kudhulumu dadake kimapenzi

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAMUME ameshtakiwa kwa kushirikiana na rafikiye kumficha dadake mwenye umri wa miaka 17, na kuishiwa kudhulumiwa kimapenzi.

Elly Ochieng Oyoo alishtakiwa kwa kuficha maafisa wa usalama kwamba rafiki yake Alloys Ouma alikuwa amemficha msichana huyo katika makazi yao mtaani Sabasaba, Kaunti Ndogo ya Embakasi, Nairobi.

Ochieng, 27 alishtakiwa mbele ya hakimu mkazi Eric Mutunga.

Hakimu alielezwa Oyoo alijua rafikiye Alloys alikuwa amehepa na msichana na kumficha katika makazi yao na kumdhulumu kimapenzi.

Oyoo alikana alificha habari hizo kumsaidia Alloys asishtakiwe kwa utekaji nyara ambao adhabu yake ni kifungo cha miaka 15 gerezani.

Alloys alidaiwa alitoroka alipopata habari polisi walikuwa wanamsaka.

Ochieng alizuiliwa hadi Mei 23, 2023 ripoti ya afisa wa urekebishaji tabia itakapowasilishwa.

Bw Mutunga ataamua ikiwa atamwachilia kwa dhamana Ochieng au la akipokea ripoti hiyo.

  • Tags

You can share this post!

Wafugaji washtakiwa kwa wizi wa mifugo Nairobi

Ashtakiwa kwa wizi wa baiskeli

T L