• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 1:15 PM
Ashtakiwa kwa wizi wa baiskeli

Ashtakiwa kwa wizi wa baiskeli

Na RICHARD MUNGUTI

MSHUKIWA wa ujambazi ameshtakiwa kwa wizi wa kimabavu baada ya kupatikana akiwa na baiskeli iliyoporwa na wahuni.

Victor Ochieng alishtakiwa mbele ya hakimu mkazi Eric Mutunga.

Ochieng alidaiwa alimnyang’anya Samson Radier baiskeli katika eneo la Darfur mtaa wa Kariobangi North mnamo Mei 2, 2023.

Radier alishambuliwa na kundi la vijana akielekea nyumbani na kunyang’anywa simu ya kiungambali, baiskeli, kitambulisho na kifaa cha maji zote za thamani ya Sh28, 999.

Wakati wa kisa hicho Radier aliumizwa.

Mshtakiwa pia anakabiliwa na shtaka la kupatikana na mali iliyoibwa au kupatikana kwa njia isiyo halali.

Ochieng alikana mashtaka dhidi yake.

Kesi hiyo itasikizwa Septemba 18, 2023.

  • Tags

You can share this post!

Ashtakiwa kwa kushirikiana na rafikiye kudhulumu dadake...

Sheria mpya: Wanaouza pombe haramu kuona cha mtema kuni

T L