• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Bangi yapatikana ikinawiri kwenye nyumba ya kifahari Eldoret

Bangi yapatikana ikinawiri kwenye nyumba ya kifahari Eldoret

NA TITUS OMINDE

POLISI mjini Eldoret wanamsaka mshukiwa wa dawa za kulevya kwa kukuza bangi ya thamani ya zaidi ya shilingi milioni moja nyumbani kwake mtaani Elgon-View.

Naibu kamanda wa polisi wa kaunti ya Uasin Gishu Zacchaeus Ng’eno alisema mshukiwa alitoroka baada ya kupata habari kwamba, polisi waligundua alikuwa akikuza na kuuza dawa hizo kupitia mfumo wa Green House.

Akizungumza na wanahabari mjini Eldoret, Bw Ng’eno alisema polisi walivamia nyumba ya mshukiwa Jumanne jioni na kung’oa mashina 129 ya bangi.

  • Tags

You can share this post!

Jack ataka kunoa chipukizi Arsenal

Utamu wa Lamu ni kutembea miguu peku ‘mguu...

T L