• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 5:17 PM
Bodaboda anayedaiwa kuua rafikiye anyakwa na kuzuiliwa

Bodaboda anayedaiwa kuua rafikiye anyakwa na kuzuiliwa

NA GEORGE MUNENE

POLISI katika Kaunti ya Kirinyaga wamemkamata mhudumu wa bodaboda anayedaiwa kumuua rafiki yake na kuutupa mwili wake kwenye shimo la majitaka.

Mshukiwa huyo alikamatwa Nanyuki na kupelekwa katika stesheni ya polisi ya Wang’uru.

Kamanda wa polisi Kaunti ya Kirinyaga, Mathew Mang’ira, alisema kuwa mshukiwa huyo atashtakiwa kwa mauaji baada ya uchunguzi kukamilika.

“Mshukiwa anazuiliwa na hivi karibuni atafikishwa kortini,” akasema Bw Mang’ira.

Stephen Murimi, 31, aliuawa katika hali tatanishi na baadaye mwili wake kutupwa kwenye shimo la taka lililo karibu na nyumba ya mshukiwa.

Polisi waliutoa mwili wake kwenye shimo hilo Alhamisi iliyopita.Mwili wa mwathiriwa ulikuwa umefungwa kwa shuka, jambo linalowafanya polisi kukisia kwamba alinyongwa na mshukiwa.

Nguo alizovaa mwathiriwa zilipatikana kwenye chumba cha mshukiwa.

Familia ya mwathiriwa ilieleza kuwa mshukiwa alimshawishi mwathiriwa aache kazi yake ili waanzishe biashara ya kuuza pombe.

Familia inashuku mshukiwa alikuwa na lengo la kumuuwa mwathiriwa na ndio maana akamhadaa ana pesa nyingi.

Mwathiriwa alijulisha familia yake kuwa alikuwa kwa rafiki yake na kuahidi kuwatembelea.

Hata hivyo, familia ya mwathiriwa iliingiwa na wasiwasi baada ya mwana wao kukosa kufika nyumbani alivyoahidi.

Waliamua kumtafuta kwa rafiki yake ambaye ndiye mshukiwa na kupitia usaidizi wa polisi wakaupata mwili wa mwana wao kwenye shimo hilo.

  • Tags

You can share this post!

TAHARIRI: Maelezo kuhusu wawaniaji wote yaanikwe wazi

DARUBINI YA UKWELI: Atwoli anapotosha kudai Ruto...

T L