• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:55 AM
Gaucho: Ni kinaya waliofanya maamuzi mabaya debeni wanataka Raila aitishe maandamano

Gaucho: Ni kinaya waliofanya maamuzi mabaya debeni wanataka Raila aitishe maandamano

NA WINNIE ONYANDO

RAIS wa Bunge la Mwananchi Calvince Okoth almaarufu Gaucho sasa anasema kwamba wananchi hawafai kumtegemea Kiongozi wa Upinzani Raila Odinga kuwatetea kupitia maandamano.

Katika mahojiano na Taifa Jumapili, Gaucho alisema kuwa Wakenya wanafaa kuteseka kabisa ndipo wajue umuhimu wa maandamano yaliyokuwa yakiendelezwa na Bw Odinga.

“Namrai Bw Odinga asijitokeze wakati huu kuongoza maandamano. Wakenya wamekuwa wakiyachukua maandamano hayo kama mzaha,” akasema Gaucho.

Gaucho ambaye alikuwa katika mstari wa mbele wakati wa maandamano ya Azimio yaliyolenga kupunguza gharama ya maisha alisema kwamba Bw Odinga amejitolea ya kutosha kutetea haki za Wakenya.

“Ni mara ngapi ameongoza maandamano kutetea masilahi ya Wakenya? Hata hivyo, wamekuwa wakisema maandamano ya Bw Odinga huleta maafa na uharibifu wa malia. Hii ndio maana Wakenya wanafaa kuumia zaidi ili iwe funzo kwao,” akaeleza Gaucho.

Haya yanajiri siku chache tuu baada ya Winnie Odinga kuwaonya Wakenya waachane na baba yake.

“Ni nyinyi mliamua kumpeleka Bondo, achana na baba yangu,” Winnie Odinga alisema kwenye mtandao wake wa kijamii mtu aliposema kuwa Bw Odinga anafaa kuwaongoza Wakenya kwenye maandamano kutokana na gharama ya juu ya maisha.

  • Tags

You can share this post!

Mke wa mwanasoka Ezekiel Otuoma adhihirisha mapenzi ya...

Serikali yamjengea chifu wa Bondo aliyechomewa nyumba...

T L