• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:50 AM
IEBC imeainisha wazi mazingira ya kituo cha kura – Chebukati

IEBC imeainisha wazi mazingira ya kituo cha kura – Chebukati

Na SAMMY WAWERU

MACHIFU na manaibu wao hawapaswi kuwa katika kituo au vituo vya kura.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), Bw Wafula Chebukati alisema Alhamisi, wakati uchaguzi mdogo kuchagua mbunge Kiambaa na diwani Muguga ukiendelea, maafisa hao wa serikali hawaruhusiwi kuwa kwenye vituo vya kura.

Hii ni baada ya wafuasi na viongozi wa mgombea wa United Democratic Alliance (UDA) John Njuguna Wanjiku kutoa malalamiko yao kwamba machifu wanatumika kisiasa.

“Nilitaja makundi sita yanayopaswa kuwa kwenye kituo cha kupiga kura na machifu si miongoni mwao. Hawaruhusiwi kuwa humo,” akasema.

Alisema hayo kufuatia kisa cha chifu mmoja Kiambaa aliyefukuzwa, akisisitiza kuingia kituoni kusimamia shughuli za kupiga kura.

Baadhi ya wagombea kiti cha ubunge Kiambaa walizua hofu kuhusu machifu na manaibu wao kuonekana vituoni.

“Mazingira ya kituo cha kura ni hadi mita 400 kutoka jengo linaloendeshewa shughuli, hivyo basi yeyote asiyepaswa kuwa humo awe nje kipimo kilichopendekezwa,” Bw Chebukati akasema.

Zimesalia saa chache vituo vya kupiga kura vifungwe ili shughuli za kuhesabu kura zianze.

You can share this post!

AU yakashifu ghasia Afrika Kusini, watu 72 wakiuawa

Hofu ya Eunice Sum kuhusu kufifia kwa kina dada Wakenya...