• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 3:46 PM
Justina Syokau asema anatafuta kijana barobaro bilionea kufunga naye harusi haraka upesi!

Justina Syokau asema anatafuta kijana barobaro bilionea kufunga naye harusi haraka upesi!

NA MERCY KOSKEI

MWIMBAJI wa nyimbo za injili Justina Syokau amezua gumzo mitandaoni kufuatia tangazo lake kwamba anasaka mchumba.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Justina alichapisha bango akidai yuko tayari kuoleka kabla ya mwaka ujao, 2024.

Kibango hicho anaonekana amekipakata katika eneo la umma, hadharani Jijini Nairobi.

Hali kadhalika, tangazo la mwimbaji Justina lina maelezo ya sifa au hulka anazosaka kwa mwanamume.

Alifichua kuwa anatafuta mume bilionea, mwenye umri wa miaka ishirini na tano.

“Niko soko tayari kuolewa kabla ya 2024. Sifa: Awe bilionea, umri wa miaka 25. Ikiwa unaona umefua dafu, nitumie ujumbe (DM),” linaeleza bango hilo.

Mama huyo wa mtoto mmoja alifichua sababu za kutaka mwanamume mdogo.

“Sitaki kuchumbiana na mzee. Nataka mtu mchanga, mwenye nguvu, na mzuri kitandani. Nataka bilionea mwenye umri wa miaka 25. Sijali kuhusu kabila au rangi yake. Mwanamume mwenye umri wa miaka 70 au zaidi hataniridhisha,” alifafanua, chapisho ambalo lilizua ucheshi Instagram.

Akitoa masharti ya mpenzi wake mtarajiwa, Justina alisema kuwa awe tayari kupata watoto naye.

Mwimbaji huyo alifichua kuwa atakuwa na timu ya wataalamu wa mahusiano watakaomsaidia kufanya mchujo, mara tu mabilionea wanaovutiwa naye watakapotuma maombi.

Justina alisema hatapoteza muda pindi atakapokutana na kibarafu wake wa moyo.

“Tutaangalia akaunti zao kubaini ikiwa ni mabilionea wa kweli na sio matapeli. Sitaki kuteseka. Maadamu awe tayari kunioa ndani ya siku tatu. Niko tayari. Siku ya kwanza anipe pete ya Almasi yenye thamani ya Sh5 milioni. Siku ya pili itakuwa malipo ya mahari nyumbani kwa wazazi wangu huko Machakos, ambayo ni Sh2 bilioni, na siku ya tatu, tunafunga ndoa ya kupendeza kwenye boti kule Dubai,” alifafanua msanii huyo anayekisiwa kuwa na zaidi ya miaka 35.

Justina alisema yuko tayari kupata watoto 10 na bilionea huyo, akisema alitaka chopa au ndege ya kibinafsi kama zawadi.

“Nimechoka kutumia magari. Sasa nataka kuruka kwa chopa au ndege binafsi. Pia anipatie mashine za bei ghali zinazomfaa mke wa bilionea,” alisema.

  • Tags

You can share this post!

Mnataka kukaa msituni hadi 2032? Gachagua akejeli jamii ya...

Mama mjamzito avuka mto hatari uliofurika akitafuta...

T L