NA BENSON AMADALA
KAMPUNI ya Sarrai Group, Uganda imeanza kukarabati vifaa vya kiwanda cha sukari cha Mumias kinachokumbwa na madeni na kuashiria mwanga wa matumaini kuhusu ufufuzi wa kiwanda hicho.
Shughuli hizo zinafanyika huku kampuni hiyo ikifuatilia kesi ya rufaa inayopinga uamuzi wa Mahakama Kuu kuondoa PVR Rao kama meneja mrasimu.