• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:50 AM
Katibu taabani kwa kula njama za kulaghai

Katibu taabani kwa kula njama za kulaghai

Na RICHARD MUNGUTI

KATIBU wa kampuni moja ya biashara ameshtakiwa pamoja na wakurugenzi wawili kwa kula njama za kumfurusha mwenzao.

Katibu huyo Victor Arara Were alishtakiwa Jumatatu mbele ya hakimu mkuu mahakama ya Milimani Bw Lucas Onyina.

Katika cheti cha mashtaka Were anadaiwa alishirikiana na Awadh Swaleh Said na Swaleh Awadh Saleh kwa kula njama za kumtimua Bw Omar Saleh Said katika kampuni ya Kilindini Warehouse (K) Limited (KWL).

Hakimu alielezwa kuwa watatu hao Said, Saleh na Were walipanga kumwondoa Omari katika kampuni hiyo ya KWL kwa kubadilisha Fomu za Hisa katika afisi za msajili wa kampuni.

Hakimu alielezwa na kiongozi wa mashtaka kwamba watatu hao walikula njama hiyo baada ya Omari kutoa mtaji wake wa hisa katika kampuni hiyo ya KWL wa Sh39.9 milioni.

Hata hivyo, Said na Saleh hawakufika kortini kama walivyoagizwa Aprili 4, 2023.

Kufuatia kutofika kwao mahakamani kujibu shtaka, Bw Anderson Gikunda aliomba mahakama itoe kibali cha kuwatia nguvuni.

Bw Onyina aliamuru polisi wawakamate na kuwafikisha kortini kujibu mashtaka.

Said, Saleh na Were wanadaiwa walikula njama za kumlaghai Omari miaka 23 iliyopita.

Were aliomba aachiliwe kwa dhamana lakini kiongozi wa mashtaka Bw Anderson Gikunda akapinga akisema “watatu hao wamewasumbua polisi sana kuwafikia.”

Mahakama iliombwa ikatae ombi la Were, kisha iamuru akae rumande hadi kesi itakapokamilika.

Were alishtakiwa alikula njama za kumlaghai Omari hisa katika KWL kati ya Desemba 1999 na Januari 2000.

  • Tags

You can share this post!

Ulevi shule za sekondari wasikitisha

Seneti yashutumu magavana wanaotumia dini kukwepa...

T L