• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 9:16 PM
Kindiki afanya mkutano muhimu Lamu kukoleza vita dhidi ya Al-Shabaab

Kindiki afanya mkutano muhimu Lamu kukoleza vita dhidi ya Al-Shabaab

NA KALUME KAZUNGU

WAZIRI wa Usalama wa Ndani Prof Kithure Kindiki anakutana na wakuu wa usalama, viongozi wa kijamii na wazee kujadili masuala ya usalama na jinsi vita dhidi ya Al-Shabaab vitakavyokolezwa Lamu.

Waziri Kindiki anakutana na wakuu wa usalama na wale wa kitengo cha ujasusi, ambapo atachukua maoni yatakayosaidia kukabiliana na ugaidi na itikadi kali.

Ziara ya Prof Kindiki pia inanuia kuzidisha ushirikiano kati ya jamii na vitengo vya usalama, ambapo hali hiyo au mazingira ya aina hiyo yanalenga kufaulisha utoaji ripoti, taarifa na habari muhimu kati ya pande hizo mbili kukabiliana na kutokomeza magaidi.

Anazuru maeneo mbalimbali ya Lamu Magharibi, ambapo pia atakutana na viongozi wa jamii mbalimbali katika kutafuta muafaka utakaohakikisha kuna umoja na utangamano mwema ili iwe rahisi kwa walinda usalama na umma kudumisha ushirikiano.

Ziara ya waziri Kindiki inajiri siku nne baada ya Rais William Ruto kuzuru Lamu na kutangaza vita vikali dhidi ya magaidi wa Al-Shabaab.

Mnamo Jumamosi, kiongozi wa taifa aliwapa mambo mawili, wahame Kenya ama wasafiri kuenda mbinguni.

  • Tags

You can share this post!

Wanne washtakiwa kwa kumjeruhi Profesa akiombea ploti yake

Tanzania yakosolewa vikali kufuatia operesheni yake ya...

T L