NA WINNIE ATIENO
GAVANA wa Kilifi, Bw Amason Kingi, amesema mkataba wake na Naibu Rais, Dkt William Ruto, ulihitaji kuwa endapo Kenya Kwanza itashinda urais, pesa zitengwe ili kufufua viwanda vya kilimo vilivyoporomoka Pwani.
Kulingana naye, mkataba huo unahitaji pia pesa kutengwa kila mwaka kununua ardhi zitakazogawiwa maskwota.
Aliwarai Wapwani kuunga mkono chama chake cha PAA ili kipate usemi kitaifa.