• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 9:50 AM
Magoha akasirishwa na maafisa wake kwa kufeli kucheza video

Magoha akasirishwa na maafisa wake kwa kufeli kucheza video

Na CHARLES WASONGA

KIOJA kilishuhudiwa Alhamisi katika Taasisi ya Kuandaa Mtaala Nchini (KICD), Nairobi, Waziri wa Elimu alipozomea maafisa wake hadharani kwa kutomakinika kazini.

Hii ni kufuatia hitilafu iliyotokea na kuchagia kutochezwa kwa kanda ya video ya kuonyesha ufanisi wa mpango wa serikali wa kutoa msaada wa masomo kwa watoto kutoka familia masikini, maarufu kama, Elimu Scholaship Programme”.

Mpango huo, ulianzishwa mwaka jana, 2020, hulenga kufaidi wanafunzi waliofanya mtihani wa kitaifa wa darasa la nane (KCPE) na kupata alama bora lakini hawawezi kupata karo.

“Nitaanza kwa kusema kuwa sijawahi kuhusishwa na utovu wa mipango ninaoushuhudia hapa asubuhi ya leo. Hali hiyo ikome kabisa! Nilitarajia maafisa wahusika kucheza video hii mapema kuhakikisha ni shwari. Sitakubali radhi zenu!”, Magoha akafoka.

Waziri huyo alisema hayo baada ya maafisa wa wizara yake kuomba radhi kufuatia video hiyo kufeli kucheza.

Lakini Profesa Magoha alisema tukio hilo iliabisha wizara yake wakati wa shughuli hiyo ambayo ilihudhuriwa na maafisa wakuu katika wizara yake na wanahabari.

Shughuli hiyo pia ilikuwa inapeperushwa moja kwa moja katika mtandao wa Facebook na You Tube ya Wizara ya Elimu.

Jumla ya wanafunzi 9,000 walipfanya mtihani wa KCPE ya 2020 walipata udhamini wa masomo chini ya mpango huo. Gharama zao zote za masomo kuanzia kidato cha kwanza hadi kidato cha nne zitalipwa chini ya mpango huo unaodhaminiwa na serikali kuu kwa ushirikiano na Benki la Dunia.

You can share this post!

Vipusa wa Zambia wapondwa 10-3 na Uholanzi kwenye Olimpiki

Vyombo vya habari vishirikiane na NLC kuripoti visa vya...