• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:50 AM
Mbarire ataka maandamano ya Azimio yazimwe

Mbarire ataka maandamano ya Azimio yazimwe

VIONGOZI wa United Democratic Alliance (UDA) walimkabili kiongozi wa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya, Bw Raila Odinga na kuiomba serikali kupiga marufuku maandamano yanayoendelea.

Wakiongozwa na mwenyekiti wa kitaifa wa UDA, Bi Cecily Mbarire, viongozi hao walisema Ijumaa kuwa maandamano hayakuwa ya amani tena na hayafai kuruhusiwa nchini.

“Maandamano yanayoongozwa na Bw Odinga yanaathiri uchumi wetu na yanafaa kukomeshwa mara moja,” Bi Mbarire ambaye pia ni Gavana wa Embu akasema.

Alisema hayo akiwa Sagana mjini, kaunti ya Kirinyaga wakati wa uzinduzi wa harakati za kuwasajili wanachama wa UDA.

  • Tags

You can share this post!

Wanajeshi waliotumwa DRC kukawia zaidi

Masuala Manne Makuu: Raila asimama kidete

T L