• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Mbunge taabani kwa matamshi yake kuhusu wenye ardhi na ugaidi

Mbunge taabani kwa matamshi yake kuhusu wenye ardhi na ugaidi

NA KALUME KAZUNGU

VIONGOZI katika Kaunti ya Lamu, wameitaka Idara ya Kuchunguza Uhalifu (DCI) imhoji mbunge Mwakilishi wa kaunti hiyo, Bi Muthoni Marubu, kuhusu matamshi yake yaliyohusisha wamiliki wa mashamba makubwa na ugaidi.

Wakati wa ziara ya Rais William Ruto kaunti hiyo majuzi, Bi Marubu alidai kuwa kati ya mashambulio ambayo yamekuwa yakitokea, mengi yalishuhudiwa katika maeneo ambapo kuna wamiliki wa mashamba makubwa.

Alidai nia yao ni kufurusha watu fulani kwa kuwatia hofu.

Seneta Maalumu, Bi Shakila Abdalla na viongozi wengine wakiwemo madiwani walimkashifu wikendi na kutaka akaeleze polisi anachojua kuhusu mashambulio hayo.

“Matamshi yake yameleta taharuki katika jamii,” akasema Bi Abdalla.

  • Tags

You can share this post!

Sh75m za ruzuku ya mafuta zilipotea kila siku – Ripoti

Raila ataja mbinu mpya za kukabili serikali ya Ruto

T L