• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Mpira wa vikapu kurejea viwanjani Juni 12-13, ratiba imetangazwa Jumatatu

Mpira wa vikapu kurejea viwanjani Juni 12-13, ratiba imetangazwa Jumatatu

Na GEOFFREY ANENE

SHIRIKISHO la Mpira wa Vikapu (KBF) limetangaza ratiba ya mechi za Ligi Kuu na Ligi za Daraja za Pili za wanaume na wanawake zitakazorejea Juni 12-13 kwa mara ya kwanza tangu Machi.

Ligi hizo zilisimamishwa kwa ghafla Machi 26 kufuatia tangazo la Rais Uhuru Kenyatta la kusitisha shughuli zote za michezo ili kupunguza kuenea kwa virusi vya corona.

Marufuku dhidi ya michezo iliondolewa Mei 1, ingawa mashirikisho mbalimbali yamekuwa yakijipanga kabla ya shughuli kurejea.

Chuo Kikuu cha Nairobi kitakuwa mwenyeji wa mechi za wikendi hii. Mabingwa wa zamani wa Ligi Kuu ya Wanawake Eagle Wings watakuwa wa kwanza kujibwaga uwanjani dhidi ya wenyeji UoN Dynamites.

Nayo, Blades ya Chuo Kikuu cha Strathmore itashuka uwanjani kuzichapa dhidi ya timu ya Chuo Kikuu cha Kenyatta maarufu Pirates katika Ligi Kuu ya Wanaume.

RATIBA:

Juni 12

Ligi Kuu ya Wanawake – Eagle Wings vs UoN Dynamites, Zetech vs Storms, Africa Nazarene vs KU Oryx; Ligi Kuu ya Wanaume – Blades vs KU Pirates, Equity Bank vs EMYBA; Ligi ya Daraja ya Pili ya Wanawake – JKUAT vs Safe Spaces; Ligi ya Daraja ya Pili ya Wanaume – NEOSASA vs JKUAT, Nets vs Mustang

Juni 13

Ligi Kuu ya Wanawake – UoN Dynamites vs Storms, Eagle Wings vs Equity Bank, Africa Nazarene vs Zetech; Ligi Kuu ya Wanaume – EMYBA vs Equity Bank, Ulinzi Warriors vs UoN Terror; Ligi ya Daraja ya Pili ya Wanaume – Moi Air Base vs Nets, Little Prince vs Trailblazers, NEOSASA vs Mustang.

  • Tags

You can share this post!

Mkimbizi Msafiri akimbia kilomita zaidi ya kilomita 500...

Mama mpiganaji wa Mau Mau aeleza dhuluma walizopitia