• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Mshukiwa wa mauaji azuiliwa siku 14 Juja

Mshukiwa wa mauaji azuiliwa siku 14 Juja

Na LAWRENCE ONGARO

MAHAKAMA ya Thika imeamuru mshukiwa Evans Karani azuiliwe katika kituo cha polisi cha Juja kwa siku 14 zaidi ili uchunguzi wa mauaji ya mpenziwe ukamilishwe.

Inadaiwa kuwa mnamo Aprili, 14, 2021, katika kijiji cha Witeithie mshukiwa alimuua Catherine Nyokabi baada ya kutofautiana kuhusu mapenzi.

Hakimu mkuu wa Thika Bw Oscar Wanyanga, aliamuru mshukiwa azuiliwe katika kituo cha polisi cha Juja kwa siku 14 ili uchunguzi ukamilishwe.

Hakimu pia aliamuru mshukiwa afanyiwe uchunguzi wa kiakili ili kubainisha iwapo ana akili timamu.

Aliongeza kusema kuwa mawasiliano ya simu yatafuatiliwa kupitia kampuni ya mawasiliano ya Safaricom ili kupata maelezo kamili ya “ni watu gani waliwasiliana nao kabla na baada ya mauaji hayo”.

Mshukiwa alipoulizwa iwapo ana jambo lolote la kusema kuhusiana na uamuzi huo alisema angetamani kesi hiyo iharakishwe ili aanze kutumikia kifungo chake mapema.

Kesi hiyo iliendeshwa kwa njia ya mtandao huku mshukiwa akijibu mashtaka akiwa katika kituo cha polisi cha Juja.

Kesi hiyo itatajwa tena mnamo Mei, 3, 2021, baada ya mshukiwa kufanyiwa uchunguzi wa akili.

Mwili wa marehemu Catherine Nyokabi, ulihifadhiwa katika chumba cha maiti cha City jijini Nairobi.

You can share this post!

Seneti yaondolea KNH lawama kuhusu kifo cha Walibora mauko...

Wito kwa walemavu wajiunge na miradi ya maendeleo