• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 2:55 PM
Mukhisa Kituyi asema atagombea urais

Mukhisa Kituyi asema atagombea urais

Na BRIAN OJAMAA

KATIBU Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na ustawi (UNACTAD) Dkt Mukhisa Kituyi ametangaza kwamba atagombea urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2022.

Dkt Kituyi anajiunga na viongozi wengine kama Naibu Rais William Ruto, kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga, Musalia Mudavadi wa chama cha Amani National Congress na Kalonzo Musyoka wa Wiper ambao wametangaza azima ya kugombea urais kumrithi Rais Uhuru Kenyatta.

Akizungumza na wanahabari mjini Bungoma Jumamosi, Dkt Kituyi alisema kwamba, kwa muda ambao amehudumu katika Umoja wa Mataifa, amepata tajiriba ya kumwezesha kuongoza Kenya.

“Sio siri tena, nitagombea urais kwenye uchaguzi wa 2022, hakuna anayefaa kutuagiza tuunge fulani mkono. Tunahitaji Rais atakayeokoa nchi hii kutoka kwa mateso yanayoletwa na uchumi mbaya,” alisema.

Alisema lengo lake la kugombea urais ni kutatua matatizo ya Wakenya na kuimarisha uchumi.

You can share this post!

Masharti makali shuleni

Baadhi ya watumiaji mitandao ya kijamii wakosoa Uhuru...