• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 11:53 AM
Mwanamume aliniomba penzi, kabla sijamjibu asharukia na kuanza kutongoza rafiki yangu!

Mwanamume aliniomba penzi, kabla sijamjibu asharukia na kuanza kutongoza rafiki yangu!

SHANGAZI;

Kuna mwanamume anayenitaka kimapenzi. Nampenda lakini nimemwambia anipe muda nifikirie kwani sitaki ahisi amenipata kwa urahisi. Sasa ameanza kumtongoza rafiki yangu. Nifanyeje?

Inaonekana mwanamume huyo anahitaji mpenzi haraka na ndiyo sababu amehamia kwa rafiki yako. Kama kweli unampenda, ni heri ukubali tu kwa sababu rafiki yako akimkubali utamkosa.

Nilipata mtoto nje, sasa mamake ataka kumleta sijui nitaambia nini mke

Nililikuwa na mpango wa kando lakini tukaachana. Tulizaa mtoto pamoja na sasa anatishia kumleta kwangu. Sijui nitamwambia nini mke wangu. Nifanye nini?

Huyo ni mtoto wako na huwezi kumkana. Ulishiriki mapenzi nje ya ndoa ukijua ni makosa. Sasa wakati umewadia kwako kuwajibika kwa kitendo chako. Mimi sina ushauri wowote kwako. Jipange.

Miaka 3 sasa na hajanipa tunda, nahisi hanijali

Kulingana na ushauri wako, mapenzi ya dhati ni mtu kumjali mwenzake. Nimekuwa na mpenzi kwa miaka mitatu lakini amenikataza kabisa kuonja asali. Anasema ananipenda lakini nahisi hanijali. Waonaje?

Ndio, mapenzi ya dhati ni mtu kumjali mwenzake. Lakini mapenzi hayamaanishi tendo la ndoa. Ninaamini mpenzi wako amekupa sababu ya msimamo wake. Kama unampenda na kumjali, heshimu uamuzi wake.

Mume wangu ni mzee kuniliko, naona aibu kutembea naye hadharani, watu watatusema

Mpenzi wangu ni mwanamume ambaye nimemzidi umri kwa miaka mingi. Naona aibu kutembea naye hadharani kwa sababu ya tofauti yetu ya amri na nina hakika watu wanatusema. Naomba ushauri wako.

Kama unataka kuishi maisha ya kuridhisha nafsi yako, usiogope kusemwa. Watu watakusema tu hata uwe na tabia ya malaika. Huyo ndiye chaguo la moyo wako. Waache waseme mwishowe watachoka.

  • Tags

You can share this post!

Wakulima wasambaziwa mbegu za alizeti kusaidia kupunguza...

Brian Mwenda anayedaiwa kuwa ‘wakili feki’...

T L