• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Mwanamume asukumwa jela miaka 25 kwa kuua mtoto

Mwanamume asukumwa jela miaka 25 kwa kuua mtoto

Na BRIAN OCHARO

MWANAMUME amehukumiwa kifungo cha miaka 25 gerezani baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya mtoto mwenye umri wa miaka 11.

Manfred Otieno Odhiambo, 40, alipatikana na hatia kwa kosa ambalo alifanya miaka sita iliyopita katika mtaa wa Likoni, Kaunti ya Mombasa.Jaji Dorah Chepkwony wa Mahakama ya Mombasa alisema ilithibitishwa mshukiwa huyo alitenda tendo la kinyama kwa mtoto mdogo.

Mahakama ilitupilia mbali ombi la Bw Odhiambo aliyetaka kuachiliwa akisema ana familia inayomtegemea.Mshukiwa huyo hata hivyo alishikilia kuwa hakuhusika katika mauaji hayo na kulaumu familia ya mwendazake kwa kumsingizia.

Kiongozi wa Mashtaka, Bi Vallerie Ongeti alitaka mshukiwa huyo kufungwa jela maisha.Familia ya msichana huyo hawakuridhishwa na uamuzi uliotolewa wakamwomba Kiongozi wa Mashtaka ya Umma Noordin Haji kukata rufaa.

“Tulitarajia kuwa angepewa miaka 40 au kufungwa jela maisha. Alikata maisha ya mtoto ambaye hakuwa na hatia. Sijafurahia kifungo hicho,” alisema Bi Pauline Njeri, mamake marehemu.

Odhiambo alishtakiwa kwa mauaji ya Stella Wangui, ambaye alikuwa mwanafunzi katika shule ya msingi ya Bethsaida. Mahakama iliambiwa alificha mwili wake mvunguni mwa kitanda.

  • Tags

You can share this post!

EPL kutuza vikosi vyenye idadi kubwa ya wanasoka...

Kalonzo awarai vinara wa OKA kumpa tiketi kuwania urais 2022