• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Mwanaume niliyemkataa amenitusi eti nina kisima kisichovutia yeyote. Nishauri

Mwanaume niliyemkataa amenitusi eti nina kisima kisichovutia yeyote. Nishauri

SHANGAZI;

Mwanamume niliyemkataa amenitumia ujumbe ambao umenichoma sana moyoni na kunifanya nijichukie. Eti amesikia kisima changu ni kirefu hakuna anayeweza kuchota maji humo. Nifanyeje?

Hatua ya mwanamume huyo inatokana na machungu ya kumkataa. Unafaa kumjibu ili ahisi kama wewe. Mwambie ulimkataa baada kuambiwa kuwa mkono wake ni mfupi sana hauwezi kufikia kisima chochote.

Mke hutembelea mganga ilhali sisi ni Wakristo

Nimegundua mke wangu amekuwa akitembelea mganga maarufu kwa wanawake walio na matatizo katika ndoa zao. Sielewi kwa sababu ndoa yetu ni thabiti. Isitoshe, sisi ni watu wa kanisa. Nina wasiwasi.

Inawezekana mke wako amepotoshwa na marafiki washirikina. Zungumza naye ujue sababu na ikiwezekana ushirikishe viongozi wa kanisa kumtoa katika imani hiyo potovu.

Nahofia nikimwonjesha asali ataacha kunipenda

Nimekuwa na mpenzi kwa miezi kadhaa na anataka kuonja asali. Nampenda sana na sitaki kumpoteza. Mpenzi wangu wa kwanza aliniacha baada ya kuchovya. Nifanye nini?

Mapenzi ni kama mchezo wa karata. Mpenzi wako anaweza kuonja kisha akuache ama akupende zaidi. Akiamua kukuacha huwezi kumzuia. Kama hutaki hawezi kukulazimisha. Uamuzi ni wako.

Nafikiria kuoa mwanamke aliyeachana na rafiki yangu

Rafiki yangu aliachana na mke wake majuzi baada ya kuishi pamoja kwa miaka miwili. Nilikuwa nikimtaka kabla hajamuoa na bado nina hisia kwake na ninajua atanikubali. Waonaje?

Sioni shida yoyote hapo. Mwanamke huyo sasa yuko huru kuolewa na mtu mwingine. Huenda rafiki yako hatafurahia hatua yako hiyo. Lakini maisha yako ni muhimu kuliko urafiki. Akikubali mpango wako mchukue.

  • Tags

You can share this post!

WANDERI KAMAU: Kawira Mwangaza ni mwathiriwa wa mitazamo...

Tambua kwa nini ‘kabeji za kichina’ ndio mpango mzima...

T L