• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 3:46 PM
Nafikiria kumwambia baba simpendi mke wake wa pili

Nafikiria kumwambia baba simpendi mke wake wa pili

SHANGAZI;

Nina miaka 22. Wazazi wangu waliachana na baba akaoa mke mwingine. Mke wake huyo hanipendi na ananitesa. Nafikiria kumwambia baba lakini pia sitaki wagombane kwa ajili yangu. Nishauri.

Kulingana na umri wako, wewe sasa ni mtu mzima na muda si mrefu utatoka katika familia hiyo ukaishi kwako. Badala ya kuzua ugomvi kati yao, ni heri uvumilie hadi wakati huo.

Ataka nipunguze uzito, nisome zaidi ili tuoane

Mpenzi wangu amenipa masharti mawili kabla ya kumuoa. Kwanza anasema mimi ni mkubwa sana kwa hivyo nipunguze mwili kupitia mazoezi ya kila siku. Pili anataka nirudi chuoni kwa masomo zaidi.

Mpenzi wako anakutakia mema na yote hayo yanawezekana. Mwili kiasi na mazoezi ni muhimu kwa afya yako. Masomo zaidi yanatakuongezea ujuzi wa kazi na kukuletea mapato zaidi. Zingatia ushauri wake.

Sijui kama mpenzi atakubali mwanaume aliyenitaka anipe kazi

Nina miaka 28, na ninatafuta kazi. Mwanamume aliyekuwa akinitaka kimapenzi ni mkubwa wa kampuni fulani na yuko tayari kunipa kazi. Mpenzi wangu anamjua na sijui kama atakubali. Nishauri.

Kama mpenzi wako anakuamini, hafai kukukataza kuchukua kazi hiyo eti kwa sababu mwanamume huyo alikuwa anakutaka. Isitoshe hajakuwekea sharti la kuwa mpenzi wake ndipo akupe kazi. Shauriana naye.

Nafikiria kuacha elimu chuoni nisaidie wazazi kuendesha biashara yao

Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu. Wazazi wangu wanafanya biashara. Nafikiria kuacha masomo ili niwasaidie kwa sababu wadogo zangu pia wako shuleni. Waonaje?

Nia yako ya kusaidia wazazi kazi ni nzuri. Lakini kumbuka kuwa hiyo ni biashara yao si yako. Wamejitolea kukusomesha ili nawe ujitafutie mali yako. Kama bado wana uwezo wa kuendesha biashara yao, shughulika na masomo yako.

  • Tags

You can share this post!

Hisia mseto zaibuka baada ya Mwangaza kuokolewa na Seneti

Koffi Olomide kutumbuiza nchini akiendelea kusahau masaibu...

T L