NA MWANGI MUIRURI
TABIA ya maafisa wa polisi vijana kupenda mitandao ya kijamii sasa inahatarisha taaluma za wakubwa wao katika Eneo la Kati.
Aidha, tabia hiyo imelaumiwa kama kiini cha idadi kubwa ya maafisa hao wachanga kusahau kumakinika kazini na kutotunza silaha zao hivyo kuwarahisishia wahalifu kazi ya kuwapokonya.
Kati ya Februari 25 na Machi 11, majambazi wamewapokonya polisi wawili silaha katika Kaunti ya Murang’a.