• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Sheria ya Fedha 2023 kuanza kutekelezwa

Sheria ya Fedha 2023 kuanza kutekelezwa

NA RICHARD MUNGUTI

WAKENYA sasa wataanza kutozwa ushuru kwa lazima baada ya Mahakama ya Rufaa kufutilia mbali agizo la kuzima utekelezaji wa Sheria ya Fedha, 2023 lililotolewa na Mahakama Kuu mnamo Juni 30, 2023.

Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa wamesema serikali imekumbwa na shida ya kulipa mishahara.

Waziri wa Fedha Profesa Njuguna Ndung’u aliwasilisha rufaa kupitia kwa Mwanasheria Mkuu Justin Muturi kupinga agizo la Juni 30, 2023 la kupiga breki sheria hiyo tata.

Majaji Mohammed Warsame, Kathurima M’Inoti na Hellen Omondi kwenye agizo lao wamesema Sheria ya Fedha ina siku 90 ambapo zikitamatika, mzunguko mwingine wa bajeti unaanza.

  • Tags

You can share this post!

Chira atiwa mbaroni

Mzozo wa Magic Business Centre ulituumiza – wapangaji

T L