Na FRANKLIN MUKEMBUKAJUKI-NITHI
BAADA ya uteuzi wa wanafunzi wa darasa la nane wanaojiunga na Kidato cha Kwanza kuanzia Agosti, kumekuwa na malalamishi miongoni mwa wazazi, walezi na hata wanafunzi wengine wakidai hawakupewa nafasi katika shule walizozichagua.
Ukweli ni kwamba, sio rahisi wanafunzi wote kupata nafasi katika shule walizozichagua. Wanafunzi wangependa shule fulani kuliko nyingine lakini Wizara ya Elimu ilijaribu kusawazisha uteuzi huo ili wanafunzi kote nchini wanufaike.
Itakuwa vyema wadau wa elimu wahakikishe miundo msingi katika shule zetu imeboreshwa ili kuwavutia wasomi, wazazi na walezi ndipo tuweze kujivunia kuwapeleka watoto wetu.Kila mzazi angependelea mtoto wake ajiunge na shule maarufu nchini lakini hili haliwezekani kwa kuwa wanafunzi wanaofanya KCPE nao ni wengi mno.