• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:21 PM
TANZIA: Mbunge afariki baada ya kugongwa na pikipiki

TANZIA: Mbunge afariki baada ya kugongwa na pikipiki

NA MANASE OTSIALO

MBUNGE wa Banisa Kullow Maalim Hassan alifariki Jumanne jioni alipokuwa akitibiwa katika hospitali moja jijini Nairobi baada ya kugongwa na pikipiki.

Mmoja wa jamaa zake, Bw Mohamud Haji amesema mbunge huyo aligongwa na pikipiki katika eneo la Capital Centre na akapelekwa katika hospitali ya Reliance iliyoko South C kabla ya kuhamishwa hadi hospitali ya Aga Khan.

Mbunge huyo alikuwa akihudumu muhula wake wa pili. Mwaka 2017 aliingia bungeni kupitia tiketi ya chama cha Economic Freedom Party (EFP) na mwaka 2022 alitetea kiti chake kupitia United Democratic Movement (UDM).

Mnamo Machi 20 alikuwa Mandera ambako kulikuwa kunazinduliwa ripoti ya hali ya afya katika kaunti hiyo.

Ameacha wajane watatu na watoto 16.

Atazikwa jijini Nairobi kwa kufuata kanuni za dini ya Kiislamu.

  • Tags

You can share this post!

TAHARIRI: Ni fedheha wanasiasa kufadhili wahuni

Wanakuza Hass Avocado kuwafaa wakazi wa Gusii

T L