NA EVANS JAOLA
WAKAZI wa Keiyo eneobunge la Kwanza katika Kaunti ya Trans Nzoia wameandamana Ijumaa wakipinga kuteuliwa kwa naibu chifu ambaye wanasema si mwenyeji.
Maandamano hayo yamesababisha wasiwasi Trans Nzoia na katika kaunti jirani ya West Pokot.
Kamishna wa Kaunti Gideon Uyagi amesema suala hilo linashughulikiwa kuzima mgogoro unaoshuhudiwa.