NA SHABAN MAKOKHA
WANAHABARI kutoka Kakamega jana, Jumamosi Septemba 16, 2023 walifurushwa na usimamizi wa shule ya upili ya Sacred Heart Mukumu Girls baada ya bweni moja katika shule hiyo kuteketea.
Wanafunzi, walimu na wafanyakazi wa shule hiyo waliwafurusha wanahabari wakidai kuwa wanapeperusha habari zisizofaa.
Bweni hilo lilishika moto mwendo wa saa 10.30 asubuhi Jumamosi na kama kawaida, wanahabari walienda shuleni ili kuripoti kisa hicho.
“Hatutaki wanahabari, hatutaki picha, hatutaki kamera,” wanafunzi wa shule hiyo walisema.
Shule hiyo imekumbwa na masaibu ikiwa ni pamoja na mlipuko wa ugonjwa uliowafanya wanafunzi watatu na mwalimu kufa.