NA DERICK LUVEGA
WAZIRI wa Elimu Ezekiel Machogu amewasili katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Sacred Heart Mukumu ambayo kwa zaidi ya mwezi mmoja imekuwa na visa vya wanafunzi kulazwa baada ya kuhara, kutapika na kuumwa na tumbo.
Wanafunzi wanne walipoteza maisha. Vile vile mwalimu alifariki dunia baada ya viungo muhimu kukataa kufanya kazi. Vifo vya watano hao vinahusishwa na ulaji wa chakula kibovu na unywaji wa maji machafu.
Waziri Machogu anatarajiwa kufungua kituo cha usafishaji maji shuleni humo.
Wanafunzi watakuwa wakinywa maji safi yaliyopitia katika mtambo wa kisasa wa kuondoa vimelea na uchafu mwingine.