NA FARHIYA HUSSEIN
WAKAZI wa Kilifi wamepata afueni baada ya kaunti hiyo kufungua mahakama.
Hapo awali, wakazi walilazimika kutafuta huduma za mahakama nje ya Kilifi.
Akifungua rasmi asasi hiyo, Gavana wa Kaunti hiyo, Bw Gideon Mungaro alisema lengo lao kuu kama serikali ni kutatua suala la mrundiko wa kesi, ambayo imekuwa changamoto kubwa katika mahakama.
“Tunalenga kuanzisha mahakama za kaunti katika kila eneobunge, na tayari tumetenga Sh50 milioni,” alisema Gavana.