• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 7:55 AM
Mwanamume apatikana amefariki ndani ya chumba kwenye orofa ya nne Riviera Court

Mwanamume apatikana amefariki ndani ya chumba kwenye orofa ya nne Riviera Court

Na SAMMY KIMATU

MWANAMUME, 27 apatikana akiwa amefariki katika nyumba yao siku tano baada ya tukio sawa na hilo kutokea katika tarafa ya South B, Kaunti ya Nairobi.

Kisa hili kilitokea katika chumba nambari 401, orofa ya nne katika Riviera Court mtaani Plainsview, kaunti ndogo ya Starehe.

Awali, Bw Musyoka Mutinda, 45 alipatikana amefariki kitandani nyumbani kwake katika eneo la Budalangi lililoko kwenye mtaa wa mabanda wa Mukuru-Kayaba.

Akithibitisha kisa hicho, mkuu wa polisi eneo la Makadara, Bw Timon Odingo alisema maafisa kutoka idara ya DCIO wanachunguza kilichosababisha vifo katika visa vyote viwili.

“Katika visa hivi viwili, tunachukulia kama ni matukio ya vifo vya ghafla. Hata hivyo, wapelelezi kutoka idara ya DCIO watachunguza ili kubaini kilichosababisha kifo cha wanaume wawili katika kaunti ndogo ya Makadara,” Bw Odingo akanena.

Fauka ya hayo, ripoti ya polisi ilisema marehemu, Bw Solomon Musembi aliyekuwa na umri wa miaka 27 alipatikana amefariki wakati dadake alienda kumuona kwa lengo la kumwambia anywe chai kabla ya kuenda kazini.

“Wanakaa nyumba moja na dadake, Bi Anne Ndunge. Dadake alirauka kutengeneza chai kabla ya kuenda kazini. Alipomwamsha anywe chai kabla ya kuelekea kazini, alipata kakake amekwisha kukata roho,” Bw Fredrick Otieno, anayesimamia Jumba la Riviera Court akaambia Taifa Jumapili.

  • Tags

You can share this post!

JAMVI: Chama cha Kingi hatarini kufungiwa nje kura ijayo

Akiri kuua mkewe kwa kuambiwa hajiwezi chumbani

T L