• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 10:50 AM
Chomelea ashtakiwa kwa kumpachika tineja mimba

Chomelea ashtakiwa kwa kumpachika tineja mimba

NA JOSEPH NDUNDA

MWANAMUME anayefanya kazi ya kuchomelea vyuma ameshtakiwa jijini Nairobi kwa kumpachika tineja mimba.

Omar Asman Malala, 35, jana Ijumaa alifikishwa mbele ya Hakimu Mwandamizi Gerald Mutiso katika Mahakama ya Makadara ambapo alikanusha kufanya makosa aliyosomewa.

Mahakama ilimwachilia kwa dhamana ya Sh300,000.

“Kesi hii itatajwa Septemba 11, 2023, ambapo utaratibu wa kesi utatolewa,” amesema Bw Mutiso akimwachilia Malala.

Mahakama ilielezwa kwamba mshukiwa amekuwa akimshawishi msichana wa umri wa miaka 14, anayeishi na wazazi wake, kuhepa na kuenda kumtembelea ambapo alifanya mapenzi naye.

Malala alishtakiwa kwa kukiuka kipengee cha 8 (1) cha Sheria ya Dhuluma za Mapenzi ya mwaka 2006.

Inadaiwa mshtakiwa alimfanyia N.A.M dhuluma za mapenzi kati ya Julai 1 na Agosti 18 katika nyumba yake mtaani Kayole, Nairobi.

Pia anakabiliwa na shtaka la kumfanyia mtoto kitendo cha aibu kwa kumshikashika sehemu za siri akijua ni kinyume cha sheria.

Malala alikamatwa na baadhi ya majirani waliokuwa wameambiwa kuwa msichana huyo amekuwa na mazoe ya kuhepa nyumbani kwao na kuenda kulala na mshtakiwa.

Majirani hao walimwambia msichana awapeleke nyumbani kwa Malala na wakamkamata Agosti 19, 2023.

Inadaiwa Malala alimfanyia msichana huyo kitendo hicho usiku uliotangulia.

Msichana aliambia polisi wanaochunguza kisa hicho kwamba alitumia simu kuwasiliana na Malala hadi saa tano za usiku mnamo Agosti 18, 2023, na kisha akahepa mamake alipokuwa amelala na kufululiza hadi kwa lango kuu la makazi ya mshukiwa aliyekuja kumchukua.

Mshtakiwa alimbeba kwa pikipiki hadi kwa nyumba yake wakalala pamoja na ilipofika asubuhi, mwanamume akamwambia msichana atoke kwa sababu naye alikuwa akienda kazini.

Msichana alitoka saa tatu asubuhi na kuanza kurandaranda mtaani hadi saa kumi jioni. Majirani walipomuona, walimpeleka kwa chifu na wazazi wake wakaitwa.

Walimwambia chifu kwamba tayari walikuwa wameripoti kwa kituo cha polisi cha Kayole kwamba binti yao alikuwa ametoweka.

Ni hapo ndipo msichana huyo aliwapeleka wazazi, jamaa na majirani hadi kwa Malala na akakamatwa na kupelekwa kwa kituo cha polisi cha Kayole.

Msichana alipelekwa kwa hospitali ya Mama Lucy Kibaki na alifanyiwa vipimo na ikapatikana alikuwa mjamzito.

  • Tags

You can share this post!

Jinamizi la ahadi Ruto akizuru Magharibi

Raila amsherehekea Mama Ida kwa mtindo katika hoteli ya...

T L