• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:55 AM
Gavana akanusha watoto 5 walifariki umeme ulipopotea

Gavana akanusha watoto 5 walifariki umeme ulipopotea

NAGEORGE MUNENE

GAVANA wa Embu, Cecily Mbarire, amekanusha madai kuwa watoto watano walifariki katika hospitali ya rufaa ya kaunti kutokana na ukosefu wa jenereta kufuatia kupotea kwa umeme nchini kote mnamo Ijumaa.

“Nimevutiwa na habari katika mtandao wa Twitter zinazodai kuwa watoto watano waliaga hospitalini. Habari hizi si za kweli na ni za kupotosha,” alisema.

Kulingana na rekodi kutoka hospitali hiyo, ni mtoto mmoja tu aliyezaliwa kabla ya wakati wake ambaye aliaga dunia.

“Hospitali ina jenereta tano za kutumiwa kwa dharura na kupotea kwa stima hakukutatiza shughuli,” alisema Bi Mbarire.

  • Tags

You can share this post!

Gatundu Kusini: Wahalifu wanaolenga vichwa vya watu kwa...

Atwoli asifu Rais Ruto kwa ‘kufanya maisha ya Kenya kuwa...

T L