NAGEORGE MUNENE
GAVANA wa Embu, Cecily Mbarire, amekanusha madai kuwa watoto watano walifariki katika hospitali ya rufaa ya kaunti kutokana na ukosefu wa jenereta kufuatia kupotea kwa umeme nchini kote mnamo Ijumaa.
“Nimevutiwa na habari katika mtandao wa Twitter zinazodai kuwa watoto watano waliaga hospitalini. Habari hizi si za kweli na ni za kupotosha,” alisema.
Kulingana na rekodi kutoka hospitali hiyo, ni mtoto mmoja tu aliyezaliwa kabla ya wakati wake ambaye aliaga dunia.
“Hospitali ina jenereta tano za kutumiwa kwa dharura na kupotea kwa stima hakukutatiza shughuli,” alisema Bi Mbarire.