• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:39 PM
Oparesheni kuokoa mateka zaidi wa pasta Paul Mackenzie

Oparesheni kuokoa mateka zaidi wa pasta Paul Mackenzie

Na ALEX KALAMA

OPARESHENI kusaka mateka wa mchungaji tata Paul Mackenzie katika msitu wa Shakahola, Kaunti ya Malindi Alhamisi imeingia siku ya pili.

Aidha, oparesheni hiyo inayotekelezwa na maafisa wa polisi pia inanuwia kutafuta makaburi zaidi yanayosemekana kuzikwa miili ya wafuasi wa mhubiri huyo ambaye tayari ametiwa nguvuni.

Oparesheni hiyo inaongozwa na mkurugenzi mkuu kitengo maalum kinachoshughulikia masuala ya mauaji, Idara ya Uchunguzi wa Jinai na Uhalifu (DCI), Bw Martin Nyuguto.

Bw Mackenzie anatuhumiwa kushawishi waumini wake kufunga, bila kula wala kunywa chochote akiwahadaa kwamba wakifa wataonana na Yesu.

Mhubiri Paul Mackenzie baada ya kuachiliwa na Mahakama Kuu ya Malindi. PICHA | HISANI

Visa kadha vya maafa ya washirika waliokufa njaa, vinavyohusishwa na dini na imani hiyo potovu vimeporitiwa.

Maafisa zaidi wa askari wameongezwa kusaidia kutekeleza shughuli ya kuokoa wahanga, kutafuta makaburi.

Hali kadhalika, baadhi ya waumini wameokolewa wakiwa hali mbaya kiafya.

  • Tags

You can share this post!

Uhuru kimya Ruto akitikisa Jubilee

Mkulima Wangari Kuria ambaye amejizolea lakabu...

T L