Na ALEX KALAMA
OPARESHENI kusaka mateka wa mchungaji tata Paul Mackenzie katika msitu wa Shakahola, Kaunti ya Malindi Alhamisi imeingia siku ya pili.
Aidha, oparesheni hiyo inayotekelezwa na maafisa wa polisi pia inanuwia kutafuta makaburi zaidi yanayosemekana kuzikwa miili ya wafuasi wa mhubiri huyo ambaye tayari ametiwa nguvuni.
Oparesheni hiyo inaongozwa na mkurugenzi mkuu kitengo maalum kinachoshughulikia masuala ya mauaji, Idara ya Uchunguzi wa Jinai na Uhalifu (DCI), Bw Martin Nyuguto.
Bw Mackenzie anatuhumiwa kushawishi waumini wake kufunga, bila kula wala kunywa chochote akiwahadaa kwamba wakifa wataonana na Yesu.
Visa kadha vya maafa ya washirika waliokufa njaa, vinavyohusishwa na dini na imani hiyo potovu vimeporitiwa.
Maafisa zaidi wa askari wameongezwa kusaidia kutekeleza shughuli ya kuokoa wahanga, kutafuta makaburi.
Hali kadhalika, baadhi ya waumini wameokolewa wakiwa hali mbaya kiafya.