NA WACHIRA MWANGI
MAAFISA wa polisi leo Jumamosi wanadumisha usalama kando ya jengo lililobomoka karibu na soko la Marikiti katika Kaunti ya Mombasa.
Hakuna aliyejeruhiwa wakati jumba hilo limebomoka kwa sababu wakazi na wafanyabiashara waliondoka mapema baada ya kutahadharishwa na maafisa wa kaunti.
Maafisa walikuwa wameonya kwamba jumba hilo lilikuwa na nyufa hatari, kuashiria lingebomoka wakati wowote.