• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 1:46 PM
Achinja binti na kumla

Achinja binti na kumla

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAFUNZI wa chuo kimoja kikuu amewaacha wakazi wa mji wa Kitengela vinywa wazi baada ya kumuua kinyama bintiye mwenye umri wa miaka miwili na kula viunga vya ndani vya mwanawe.

Msichana huyo mwenye umri wa miaka 24 adaiwa alijifungia ndani ya chumba chake akiwa uchi wa mnyama na kumchinja kama mnyama bintiye “huku akinena kwa lugha na ndimi sisizoeleweka.”

Majirani wa mwanafunzi huyo wa somo la biashara aliye na misuli mithili ya mwanaume walisema walishtushwa na makelele ya mtoto huyo aliyekuwa anaomba msaada.

Kisa hicho cha saa tatu usiku wa Jumapili kiliwaogofya wote waliouona mwili wa msichana huyo aliyekatwa shingo na kuondolewa viungo vya ndani na mama yake aliyezila kwa hamu kana kwamba alikuwa na njaa kuu.

Majirani waliohojiwa na Taifa Leo walisema walishtushwa na mayowe na duru aliyopiga mtoto huyo aliyeshambuliwa kwa kisu na mama yake.

Kwa pupa majirani walikimbia katika makazi ya binti huyo wakidhania kwamba amevamiwa na majmbazi.

Majirani walimkuta mwanafunzi huyo wa chuo kikuu aliyetambuliwa kwa jina Olivia Kaserran amejifungia ndani ya nyumba yake.

Wakati mwanahabari wa Taifa /Nation alifika mahala pa kisa hiki cha kutamausha, wakazi walifyata ndimi huku wachache wakidai wazazi wao hawakuwa nyumbani kilipotendeka.

Wadokezaji walisema babaye Olivia ni mwalimu katika eneo la mashariki na mama yake alikuwa ametembelea jamaa zake kaunti ya Nyahururu.

Mama yake OIivia anadaiwa alimwacha katika makazi yao punde tu alipotoka Meru na bintiye Jumamosi.

Olivia alikuwa anaishi Meru na bintiye.

“Mama huyo mwenye umri mdogo alikuwa uchi wa mnyama. Alimlaza bintiye akiwa uchi sakafuni kisha akamchinja akizugumza kwa ndimi na lugha,” alisema jirani.

Olivia alimkatakata bintiye kisha akaanza kula viungo vya ndani.

Hadi pale walivunja mlango tayari Olivia alikuwa amemuua bintiye.

Alianguka na kuzirai kando ya maiti ya bintiye.

Video zilionyesha maiti ya mtoto huyo.

Polisi walisema walipofika katika makazi hayo tayari mtoto huyo alikuwa ameaga na mama yake alikuwa amezirai

Viti na vifaa vya elektroniki katika chumba cha mazugumzo vilikuwa vimetapakaa kwote.

Polisi pia walipata kisu kilichotumika kumuua mtoto huyo.

Mshukiwa huyo alitiwa nguvuni na kupelekwa hospitali ya kaunti ndogo ya Kitengela.

Maiti ya mtoto huyo ilihifadhiwa katika mochari ya hospitali hiyo.

Jumatatu alasiri Olivia alipata nafuu na kupelekwa kuzuiliwa katika kituo cha polisi Kitengela kuhojiwa.

Taifa leo ilifaulu kumhoji mshukiwa katika hospitali ya Kitengela kabla ya kupelekwa kituo cha polisi cha Kitengela.

Akiwa amesuka nywele, mshukiwa huyo alifichua kwamba alitekeleza uhalifu huo kwa sababu ya kujichukia.

Aliambia Taifa Leo, “Ninajichukia mwenyewe. Sijipendi ndio maana niliua mtoto wangu. Nimepitia magumu na huyu mtoto.”

Pia aliongeza kusema awali alitaka kujiua mwenyewe lakini akabadilisha mawazo.

Wakati mmoja Olivia alinyamaza kabisa bila kuzugumza lakini akiwa amezama kwa mawazo.

Afisa wa uchunguzi wa Jinai Kitengela Bw Benson Mutia aliambia Taifa Leo kwamba uchunguzi umeanza kufanywa na punde tu utakapokamilika Olivia atapelekwa kortini.

Mutia alisema Olivia hajahojiwa kwa vile ameruhusiwa kutoka hospitali Jumatatu alasiri.

Kisa hiki cha kinyama kimetokea siku mbili baada ya mwanaume wa umri wa miaka 25 kumuua Gertrude Mutiso mwenye umri wa miaka 22 akidai alikuwa amemwacha na kuanza urafiki na mkubwa wao katika mkahawa wa Kitengela Pizza.

Mshukiwa alishambuliwa na wakazi waliokuwa na hasira.

Anaendelea kupata matibabu.

  • Tags

You can share this post!

Idadi jumla ya walioangamia Shakahola sasa ni 73

Wanafunzi wanufaika na sare za shule

T L