• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:55 AM
Ahadi hewa ya Raila kwa wafanyabiashara

Ahadi hewa ya Raila kwa wafanyabiashara

Na CHARLES WASONGA

MNAMO Jumatano, Machi 29, 2023, kiongozi wa Azimio la Umoja-One Kenya Raila Odinga aliahidi kuwasaidia wafanyabiashara ambao mali yao iliharibiwa wakati wa maandamano ya Machi 27.

Bw Odinga aliahidi kuwanunulia mabati, na vifaa vinginevyo kuwasaidia kujenga upya vibanda vilivyoteketezwa na waandamanaji.

Aidha, aliahidi kuwapa wafanyabiashara hao pesa za kuanzishia upya biashara zao.

“Tunasema pole kwa wafanyabiashara ambao mali yao iliharibiwa juzi katika eneo la Kibra. Tunaelewa kuwa mlipata hasara kubwa, lakini tuko tayari kuwasaidia kujenga upya vibanda vyenu kwa kuwapa mabati na pesa za kusaidia kujenga upya biashara zenu,” Bw Odinga akasema alipokutana na wafanyabiashara wa maeneo ya Makina, Karanja na Olympic.

Lakini zaidi ya mwezi mmoja baada ya Bw Odinga kutoa ahadi hiyo, wafanyabiashara hao wanalalamikia kuwa hawajapokea vifaa vya ujenzi na fedha.

Aidha, hawajapokea taarifa zozote kutoka kwa Mbunge wa eneo hilo Peter Orero au madiwani kuhusu ni lini Odinga atatimiza ahadi hiyo.

Sasa wafanyabiashara hao wanamkumbusha kiongozi huyo wa Azimio kwamba atimize ahadi yake kwani bado wanateseka.

 

  • Tags

You can share this post!

Mbwembwe mfalme akichukua usukani

Marais waalikwa wafuatilia hafla kwenye runinga

T L