• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Akaunti za M-Pesa za Pasta Ezekiel Odero zafunguliwa akisamehe waliomtesa

Akaunti za M-Pesa za Pasta Ezekiel Odero zafunguliwa akisamehe waliomtesa

Na RICHARD MUNGUTI

WAUMINI zaidi ya milioni tano wa Kanisa la Pasta Ezekiel Odero wamepata afueni baada ya kampuni ya Safaricom kufungua laini saba za MPesa za kanisa hilo zilizokuwa zimezimwa.

Agizo la kufunguliwa kwa laini hizo kulitokana na kampuni hiyo kuwapa polisi nakala za miaka sita za laini hizo.

Punde tu mahakama ilipoamuru laini hizo zifunguliwe Pasta Odero kupitia kwa wakili Danstan Omari alitangaza msamaha kwa wote waliomtesa pamoja na waumini wa kanisa lake.

Bw Omari alimweleza hakimu mkazi Ben Mark Ekhubi kwamba sasa akaunti zote 30 za kanisa hilo zilifunguliwa na ufadhili wa miradi ya kanisa unaendelea kutolewa.

Baada ya agizo kutolewa laini hizo zifunguliwe wakili Omari anayemwakilisha Pasta Odero alieleza korti “kwa niaba ya Wakristo na waumini katika kanisa la Muhubiri huyu amewasamehe wote waliomtesa.”

Wiki iliyopita akaunti za benki 30 zilizokuwa zimefungwa zilifunguliwa.

 

  • Tags

You can share this post!

Ziara za Rais ugenini raia wakikaza mshipi

Nyumba Yangu: Wanariadha kunufaika kupitia ushirikiano wa...

T L