• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Ashtakiwa kwa vitisho vya kuua

Ashtakiwa kwa vitisho vya kuua

Na RICHARD MUNGUTI

MFANYAKAZI katika kituo kimoja cha habari ameshtakiwa kwa kutisha kumuua mfanyabiashara.

Bi Farida Idris Mohamed, aliyeajiriwa na Capital FM, alishtakiwa mbele ya hakimu mkuu mahakama ya Milimani Lucas Onyina.

Farida ambaye ni mkurugenzi kitengo cha biashara, Capital FM, alikana mashtaka saba ya kumtumia Hussein Alia Amaro jumbe zenye tisho za kumuua.

Farida alishtakiwa kutekeleza kosa hilo mnamo Juni 14/15 2019.

Wakili Peter Wanyama alimwakilisha Farida.

Bw Wanyama aliomba mshtakiwa aachiliwe kwa dhamana.

Kiongozi wa mashtaka bw Anderson Gikunda hakupinga ombi hilo la mshtakiwa kuachiliwa kwa dhamana.

Katika mashtaka hayo saba mshtakiwa alimtumia Hussein jumbe hizo zenye vitisho vya kuua kupitia ujumbe mfupi, sms.

Akimwachilia kwa dhamana ya Sh100,000 pesa tasilimu, hakimu alisema dhamana ni haki ya mshtakiwa.

Kesi hiyo itatajwa baada ya wiki mbili Mei 2, 2023 kutengewa siku ya kusikizwa.

  • Tags

You can share this post!

Jambazi wa kuwekea walevi mchele ashtakiwa kwa wizi wa...

Leo ni zamu ya mawaziri Murkomen, Tuya kujibu maswali...

T L