• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 4:54 PM
Maelfu wakesha katika uwanja wa Kasarani

Maelfu wakesha katika uwanja wa Kasarani

MBWEMBWE na mihemko jana zilipamba mkutano wa Azimio la Umoja uliofanyika katika uwanja wa Kasarani jijini Nairobi ambapo kinara wa ODM Raila Odinga alitangaza rasmi azma yake ya kuwania urais 2022.

Wafuasi wa ODM na vyama vingine rafiki kutoka kila pembe ya Kenya walianza kuwasili katika uga wa Kasarani saa nane usiku wa kuamkia Ijumaa baadhi yao wakiibatiza siku hiyo ‘Sikukuu’. Hata hivyo, shughuli za kuandaa na kutayarisha maeneo ya wageni kuketi ilikuwa imeendelea usiku kucha Alhamisi kama njia ya kuhakikisha kila kitu kinakamilika kwa wakati.

Kufikia saa moja asubuhi, nusu ya uwanja huo ambao unaweza kuwapokea watu 60,000 tayari ulikuwa umejaa huku mabasi ya shule na mengine yaliyokodishwa yakiegeshwe nje ya uwanja huo pamoja na magari ya kibinafsi.

Mawaziri Peter Munya (Kilimo), Sicily Kariuki (Maji), Eugene Wamalwa (Ulinzi), Joe Mucheru ( ICT) na kiongozi wa wengi Bunge la Kitaifa Amos Kimunya ni kati ya waliohudhuria hafla hiyo

You can share this post!

Waajiri waliwapuuza wafanyakazi wakati mgumu wa Covid-19

Korti ya Juu yashikilia uamuzi kuhusu jinsia

T L