• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 8:03 AM
Maombi ya kitaifa: Mbunge Silvanus Osoro ni gwiji katika uchezaji piano

Maombi ya kitaifa: Mbunge Silvanus Osoro ni gwiji katika uchezaji piano

NA SAMMY WAWERU

MBUNGE wa Mugirango Kusini Silvanus Osoro ameonyesha umahiri wake katika uchezaji piano.

Mwanasiasa huyo mcheshi ndiye mcheza kinanda, katika maombi ya kitaifa yanayofanyika katika Mkahawa wa Kifahari wa Safaripark, Nairobi, Jumatano, Juni 7, 2023.

Maombi hayo yanaongozwa na Rais William Ruto, na yamehudhuriwa na viongozi wakuu serikalini.

Akiwa amevalia shati jeupe, suruali ndefu – long’i nyeusi na kufunga tai nyekundu yenye michirizi mieusi na mieupe, Bw Silvanus ameongoza kwaya ya bunge katika kutumbuiza hafla hiyo ya maombi.

Mbunge huyo akionekana mchangamfu, kila kundi la wanakwaya hao linapopewa fursa kuimba anacheza piano.

“Mara nyingine moja, haleluya, haleluya, haleluya…” Bw Osoro akaskika katika mojawapo ya kibao cha kutakasa akiimba, huku vidole vyake vikizama kwenye kinanda.

Osoro ndiye kiranja wa bunge la kitaifa, na katika uchaguzi mkuu 2022 alirithi wadhifa wake wa ubunge Mugirango Kusini kupitia tikiti ya United Democratic Alliance (UDA).

  • Tags

You can share this post!

Mswada wa vitisho

‘Shetani’ aingia kanisani na kutawanya na kujeruhi...

T L