• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 5:10 PM
Mhubiri Paul Mackenzie awaambia wanahabari wamnunulie angalau mkate na maziwa

Mhubiri Paul Mackenzie awaambia wanahabari wamnunulie angalau mkate na maziwa

NA ALEX KALAMA

MHUBIRI Paul Mackenzie anayedaiwa kuchangia vifo vya watu wengi katika msitu wa Shakahola, mnamo Ijumaa akiwa katika Mahakama ya Shanzu aliachilia kombora kwa wanahabari akiwataka wamnunulie angalau mkate na maziwa. 

Baada ya mhubiri huyo kudai kuwa waandishi wameunda pesa nyingi kupitia jina lake, alisikitika kwamba hawajamnunulia hata paketi ya maziwa.

“Mmetengeneza pesa sana lakini hamninunulii hata paketi ya maziwa… Si mninunulie na mimi hata paketi ya maziwa,” alisema Mackenzie.

Baadhi ya wanahabari walisikika wakiangua kicheko huku wakisema “usijali tutakununulia tu.”

Mackenzie, mkewe na watu wengine 16 walikuwa wamefikishwa katika mahakama hiyo ambapo upande wa mashtaka uliomba kupewa siku 60 zaidi za kuendelea kumzuilia mhubiri huyo tata ili kukamilisha uchunguzi wao.

Tayari maiti 243 imeshafanyiwa upasuaji na uchunguzi kubaini chanzo cha vifo vya wanaodaiwa kuwa walikuwa wafuasi wa mafundiso ya mhubiri huyo wa kanisa la Good News International.

  • Tags

You can share this post!

Msikiti wa Jamia waandaa siku ya hamasisho, Wakristo...

Manchester City watandika Manchester United na kujizolea...

T L