NA SAMWEL OWINO
MKUU wa Mawaziri Musalia Mudavadi anamtaka Rais William Ruto kushauriana na mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni ili kuwaombea msamaha Wakenya zaidi ya 41 waliofungwa jela katika taifa hilo jirani.
Bw Mudavadi ambaye vilevile ni Waziri wa Masuala ya Kigeni, amesema mbinu zote zinapaswa kutumika kuwezesha kuachiliwa huru kwa Wakenya hao.
Kauli ya waziri huyo inajiri wakati ambapo muungano wa Azimio ukiongozwa na Raila Odinga kudai serikali ya Kenya Kwanza haijui namna ya kupalilia uhusiano mzuri na mataifa jirani.