• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 9:17 PM
Niko tayari kumenyana na mradi wa Uhuru, Ruto asema

Niko tayari kumenyana na mradi wa Uhuru, Ruto asema

Na CECIL ODONGO

NAIBU Rais Dkt William Ruto amesema yupo tayari kupambana na ‘mradi’ wa Rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi mkuu wa 2022.

Japo Rais hajatangaza hadharani atakayemuunga mkono 2022, inaaminika huenda akamuunga mkono Kinara wa ODM Raila Odinga kutokana na juhudi ambazo amekuwa akifanya kumpatanisha na wanasiasa wa Muungano wa OKA.

Dkt Ruto alisema kuwa mfumo wake wa kiuchumi wa kuinua watu wa tabaka la chini tayari umemvunia uungwaji mkono wa maana kote nchini na yupo tayari kumkabili mwaniaji atakayepigiwa upatu na serikali.

“Wakenya ndio wataamua kati ya mwaniaji anayeinua maisha ya wachochole na yule ambaye ameteuliwa na watu wachache kulinda maslahi ya matajiri,” akasema Dkt Ruto kwenye makazi yake ya Karen alipokutana na viongozi wa kidini na wafanyabishara kutoka Githurai.

Alishutumu Bw Odinga kwa kujipendekeza kwa raia kupitia mfumo wa kutoa Sh6,000 kwa watu maskini, akisema enzi za kuwahadaa raia zimepitwa na wakati.

 

You can share this post!

Wakulima wa kahawa kusubiri zaidi viwanda vikarabatiwe

Atumia kahaba kuzima polo msumbufu

T L