• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 1:46 PM
Ruto: Tutajenga studio za kisasa katika kila kaunti

Ruto: Tutajenga studio za kisasa katika kila kaunti

NA WINNIE ONYANDO

RAIS William Ruto amesema serikali ya Kenya Kwanza itawasilisha mswada bungeni utakaoruhusu ujenzi wa studio za kisasa kote nchini kusaidia wasanii.

Akizungumza Jumatano wakati wa Tamasha la Muziki jijini Nakuru, Ruto alisema kwamba ameunda timu inayoongozwa na Waziri wa Michezo, Sanaa na Utamaduni Ababu Namwamba, ili kuandaa mswada huo na kuuwasilisha bungeni ndani ya miezi miwili ijayo.

Alisema kuwa serikali ina mpango wa kuimarisha sekta ya sanaa na ubunifu na hata kusisitiza kuwa tayari serikali yake imebadilisha Tume ya Kudumu ya Muziki ya Rais kuwa Tume ya Ubunifu ambayo itatimiza azma hiyo.

“Tayari tunashughulikia mswada wa ubunifu ambao utahakikisha kwamba kila kaunti itakuwa na studio ya kisasa ili kuwainua wasanii wetu,” akasema Dkt Ruto.

“Tutaendelea kushirikiana na serikali za kaunti ili tuweze kutoa fursa kwa wasanii wote, awe wa shule ya msingi au sekondari. Hatua hiyo itawasaidia kukuza talanta zao,” akaongeza Dkt Ruto.

  • Tags

You can share this post!

Ripoti zasema Yevgeny Prigozhin wa Wagner ameangamia

Oparanya anahangaishwa Mulembe wakose ujasiri kumuuliza...

T L